1

1 KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
2 Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote;
3 Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu;
4 Mwenye Kumiliki Siku ya Malipo.
5 Wewe tu tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada.
6 Tuongoe njia iliyo nyooka,
7 Njia ya ulio waneemesha, siyo ya walio kasirikiwa, wala walio potea.